+255-(0)27- 297 0056 Junction of Moshi-Arusha and Nairobi Roads rector@atc.ac.tz SMS Online Application CMU

contact info

+255-(0)27- 297 0056
Junction of Moshi-Arusha and Nairobi Roads
SMS
CMU

Post Details

VIJANA 200 WANUFAIKA NA MAFUNZO YA NISHATI JADIDIFU KUPITIA MRADI WA AJIRA KWA MAENDELEO (E4D) KATIKA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA

Vijana 200 kutoka mikoa mbalimbali nchini wamenufaika kwa kupata mafunzo ya nishati jadidifu kwenye upande wa umeme wa nguvu za Jua (Sola) yaliyotolewa na Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) kupitia mradi wa mafunzo ya kuwezesha vijana kupata ajira ili kuleta maendeleo (E4D) unaotekelezwa na shirika la Kiufundi la Ujerumani (GIZ). Akizungumza kwenye hafla ya kufunga mradi huo iliyofanyika Chuoni hapo, Afisa Biashara Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Wilfred Kawa amesema kwamba Mradi huo ulilenga kuhamasisha upatikanaji wa ajira kwa vijana ambapo mpaka sasa wameweza kutengeneza vijana 200. “Mradi huu ulilenga Zaidi kuwezesha upatikanaji wa ajira kwa vijana na kinamama hapa nchini kama mnavyofahamu kwamba tatizo la ajira ni tatizo la kidunia, kuanzia mwaka 2020 mpaka sasa tumeweza kutoa mafunzo kwa vijana 200 pamoja na kutengeneza walimu wa kutoa ujuzi wapatao 18 watakaoendelea kutoa mafunzo ya aina hii” alisema Bw. Kawa. Naye Kaimu Mratibu wa Mradi huo Mhandisi Dennis Mbangulla ameeleza kwamba “gharama za mradi huu ilikua ni Euro 235,000/- ambazo zimekwenda kwenye kazi mbalimbali ikiwemo Chuo Cha Ufundi Arusha kupitia mitaala ya kufundisha Sola na kuiboresha ifanane na mazingira ya sasa”. Kwa upande wake mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo Bw. Said Hamza ameupongeza mradi wa E4D na Chuo cha Ufundi Arusha kwa kupatiwa mafunzo hayo na kueleza kuwa kwa sasa yeye pamoja na baadhi ya wahitimu tayari wameajiriwa kwenye kampuni mbalimbali za Sola. Aidha aliomba mradi huo uendelee kufadhili mafunzo hayo kwa awamu nyingine ili watanzania wengi waweze kunufaika.

  Nov 16, 2023   |